UNATUMIA KIUNGO GANI KUTAZAMA MBALI?

8:22:00 PM Unknown 0 Comments

 
UNATUMIA KIUNGO GANI KUTAZAMA MBALI?
Mwili wa binadamu unaviungo vingi kila kimoja kikiwa na kazi yake. Ipo pia milango ya fahamu ambayo kwa kuhisi, kunusa, kuonja na kwa kuona hufanya kazi. Viungo hivi na milango hii ya fahamu si tu kwamba ipo kwa binadamu bali hata wanyama, ndege na baadhi ya wadudu wamejaliwa na Mwenyezi kuwa nayo.
Binadamu ndiye mwenye jukumu la kuwatawala ndege, wanyama, wadudu na hata viumbe wasioonekana (mapepo, majini, malaika). Kitabu cha Waebrania kimeeleza malaika ni roho wanotuhudumia, pia mzaburi amenena wazi jinsi Mungu alivyomfanya mwanadamu punde tu kama yeye na amemvika utukufu na heshima.
Licha ya utukufu huo mwanadamu si kiumbe mwenye uwezo mkubwa wa kuona. Tai, mwewe na hata ndege wengine huona mbali zaidi kuliko mwanadamu. Ni watu wachache tu wenye macho makali ya kuona mita mia tano au zaidi.
Swali, Ni kwa nini macho ya wanadamu ambao kibiblia ndio watawala wa dunia hii yanazidiwa na hawa ndege? Jibu langu ni rahisi, Mungu hakutaka mwanadamu aishi kama tai, Hakutaka mwanadamu aone mbali kwa macho ya nyama bali atumie akili, fikra na imani katika kuona kwake. Kwa njia hizi ataona mbali zaidi ya tai na hivyo atamtawala mpaka tai.
Mwanadamu anauwezo wa kuona hata miaka 20 ijayo na akanunua shamba leo na kupanda miti. Mwanadamu wa leo anaweza kuona miaka 100 ijayo. Hayati Rais Kennedy wa Marekani anayetajwa katika simulizi za kwenda mwezini, aliwaita wanasayansi wake na kuwapa wazo hilo ambalo hawakuwa wamewahi kulisikia popote. Hebu waza unamka unaitwa na Rais na anakwambia, naomba uanze kufikria jinsi gani tutakwenda kwenye Mwezi au Jua. Wakati huo wewe hujawahi hata kuzifuatilia nyota za angani.
Baada ya wanasayansi hao kufanyia kazi wazo hilo kwa miaka kadhaa walifanikiwa na kwa sasa kwenda mwezini au kutuma vyombo kwenda huko si jambo la ajabu tena. Tofauti na hayati Rais Kennedy ambaye ni mtu wa fikra, Rev Martin Luther King Jr ambaye ni mwanaharakati, yeye katika harakati zake za kumkomboa mtu dhidi ya ubaguzi  wa rangi anaonekana kuona mbali kama nabii, na hii ni kwa sababu ya Imani yake ambayo mzizi wake ni neno la Mungu.
Alisema Fred Swaniker kwamba, Afrika inahitaji Moon shoot thinking, akimaanisha tunahitaji kufikiri mbali sana, tunahitaji kuruka kifikra (kimawazo) na kutua mbali, mahali ambapo kwa uhalisia macho ya kawaida hayapaoni ila kwa imani na fikra sahihi tunapaona.
Katika ulimwengu huu hata kipofu anaweza kufanikiwa kama ubongo wake umechangamka kuliko watu mia wenye macho makali lakini ubongo umelala. Kuna jambo linanishangaza katika taifa langu, vijana wengi ukiwahoji si watu wa fikra.
Siku 1000 za kwanza katika ukuaji wa mtoto zijulikanazo kama “mwanzo bora” zina mchango mkubwa katika uwezo wa kufikri wa mtoto. Utapia mlo ndio huzaa watu wenye mawazo mgando, na mawazo maji, yote ni matokeo ya mdororo wa chakula. Mfumo wetu wa elimu hauruhusu udadisi hasa kwa kuwa mwalimu ndio kila kitu, si rahisi mfumo wetu kuzalisha watu wanaofikiri kimkakati.
Ili tupate vijana wanaofikiri sawasawa basi ni muhimu tuwajenge kwa neno la Mungu ambalo litaleta imani, tuwape chakula bora cha akili yaani vitabu sahihi vya kiada na ziada, watoto wapewe mlo kamili ukijumuisha matunda, vyakula vya wanga, protini na maji mengi.

0 comments :

Kuelekea Uhuru wa Kifedha - II

2:33:00 PM Unknown 0 Comments

 
KUELEKEA UHURU WA KIFEDHA II
(THE BIBLICAL LAWS OF MONEY)
Toleo lililopita tuliangazia kanuni moja muhimu sana ili kuelekea mafanikio ya kiuchumi katika maisha ya mtu; kanuni ya uzalishaji bidhaa au huduma. Kanuni hii huwa haimzungumziwi sana lakini ni kanuni muhimu sana kuelekea uhuru wa kifedha. Kumbuka, Fedha unazozitafuta zipo kwa watu, ili kuzipata lazima uwe na kitu cha kubadillishana (exchange). Hakuna namna utafikia uhuru wa kifedha endapo hakuna bidhaa wala huduma ambayo unaweza kutoa na watu wakakupa fedha.
Kwa mtu ambaye ameajiriwa maana yake anauza huduma, na hivyo mwisho analipwa mshahara. Mshahara unakuja kama matokeo baada ya kutoa huduma, vivyo hivyo mfanyabiashara au mjasiriamali au hata makampuni hupata fedha kutokana na bidhaa au huduma wanayozalisha.  Fedha ni matokeo ya bidhaa au huduma anayotoa mtu. Mwalimu wangu mmoja amewahi kusema, “If you don’t create or add value to others (through goods or service), you are not entitled to receive money” (Kama hauna bidhaa au huduma unayoweza kutoa kwa watu, haustahili kupokea fedha ya mtu: Tafsiri isiyo rasmi)
Mtu pekee anayeweza kuwa na uhakika wa kupata fedha bila kubadilishana na huduma au bidhaa moja kwa moja ni serikali, yenyewe inakusanya kodi. Hivyo watu watake au wasitake ni lazima serikali ikusanye fedha kutoka kwao kama kodi kwa mujibu wa sheria za nchi husika. Mimi na wewe hatukusanyi kodi, watu hawalazimiki kisheria kutupa fedha zao; hivyo basi ili kupata fedha zao lazima tuwe na kitu wanachokiitaji na kwa sababu hiyo wako tayari kukilipia ili kukipata kitu hicho. Na hapo ndipo tunapoweza kuona fedha inaingia mifukoni mwetu.
Swali unaloweza kujiuliza au unalotakiwa kujiuliza sasa, ni bidhaa gani au huduma gani unaweza kuizalisha au kutoa ambayo watu (jamii inayokuzunguka) wanahaja nayo na watakuwa tayari kuilipia ili kuipata? Iwe umeajiriwa au hujaajiriwa hili ni swali muhimu sana kama unataka kufikia uhuru wa kifedha (kutimiza mahitaji yako YOTE, na kupata ziada kwa ajili ya kufikia mahitaji mengine yanayokuzunguka; maana utamsaidiaje anayehitaji ‘chakula’ wakati hata wewe huna: Mathayo 25:37-40).
Sam Adeyemi amewahi kusema  It is not the absence of money that makes a person poor; it’s the absence of right idea (thought) that has value”. Yaani “Si ukosefu wa fedha ndio humfanya mtu kuwa masikini bali ukosefu wa wazo lenye thamani”. Hivyo kumbe fedha ni matokeo tu; yaani matokeo  ya wazo lenye thamani ambalo huzaa bidhaa au huduma; ambazo mtu hubadilishana (exchange) na fedha.
There’s a place for you at the top!

0 comments :