Mtu Jasiri

1:31:00 PM Unknown 0 Comments

MTU JASIRI
Katika ulimwengu wa sasa majasiri wengi hawajulikani. Dunia ya leo imewatukuza wasemaji ikaacha wakimya, imemdharau mtu mpole ikampa heshima mtu mkali. Katika vikao wasikilizaji wazuri hawatambuliwi kama majasiri wa kusema. Kusikiliza si jambo jepesi, hakuna mtu mgumu kumsikiliza kama mtu mkorofi na mtu asiyejua.
Si wengi wanauzoefu na uwezo wa kusikiliza kwa makini, wengi hupenda kusikilizwa si kusikiliza. Huwezi kusikiliza na huku unatazama televisheni au unasikiliza redio. Ni rahisi kuukusanya mwili lakini si akili ya usikivu. Huwezi kusikiliza ikiwa unataka kusema, unaweza kusikiliza ikiwa unataka kusikiliza. Alisema Winston Churchil, “Courage is not only what it takes to stand up and talk but courage is also what it takes to sit down and listen” kwa tafsiri “Inamhitaji mtu jasiri kusimama na kuzungumza, lakini inamhitaji mtu jasiri pia kukaa kimya na kusikiliza”.
Amenukuliwa mzee Kinana Katibu Mkuu CCM akisema, “kiongozi lazima asikilize wananchi”.  Kiongozi si lazima awe kwenye kampuni, kwenye taasisi ya umma au kwenye siasa, badala yake anaweza akawa kwenye familia baba wa familia, mama wa familia, kaka wa familia au dada wa familia.  Siku chache katika nafasi ya uongozi jambo kubwa nililojifunza ni kwamba, uongozi ni kusikiliza, It’s all about listening!
Ni raha kusikiliza, msikivu anaraha kwa kuwa anauelewa mpana. Je, ungependa kuitwa mwongeaji sana au msikivu sana. Je, ungependa mtu akitoka nyumbani kwako aseme hajawahi ona msemaji kama wewe au aseme hajawahi kukutana na mtu msikivu kama wewe.  Si vema mtu akushangae kwa kusema, “What a talker
Ni mtu jasiri peke yake anaweza kuwasikiliza waliotengwa, waliosetwa na wasio stahili katika jamii. Si rahisi kuwasikiliza wahalifu, mtu jasiri pekee anaweza kufanya hivyo.
Kwa kiongozi mpya wa nafasi na ngazi yoyote nasisitiza neno moja, sikiliza, sikiliza, sikiliza.
Tukutane kileleni wasikivu wanapopatikana.

0 comments :

Umeitwa kuongoza

10:03:00 AM Unknown 0 Comments

UMEITWA KUONGOZA
Mtu hafanyiki kiongozi kwa cheo au nafasi aliyonayo katika Nyanja za siasa, taasisi, kanisa n.k; bali ni kusudi (purpose) linalozaa maono (vision) ndani yake. Sifa kuu ya kiongozi ni kuwa na maono chanya kwa mustakabali wa anachokiongoza. Mahali ambapo hakuna maono hakuwezi kuwa na uongozi, kunaweza kuwa na cheo lakini hakuna uongozi!.
Maono ndio hufanya kiongozi awe kiongozi. Siku zote watu hawafuati mtu, wanafuata maono yake. Mahali ambapo nguvu hutumika ili kufanya watu wafuate (follow) ni kwa sababu hakuna maono yanayoshawishi watu kufuata kwa utashi na hiari yao.
Ikiwa kila mtu ameumbwa kwa kusudi maalumu, basi ni ukweli uliowazi kuwa kila mtu ameitwa kuongoza katika eneo la kusudi lake; kumbuka maono ndio yanayotengeneza kiongozi na sio kinyume chake, na maono ni picha ya kusudi ndani ya mtu. Maono ndio yaliyotengeneza mtu anaitwa mama Theresa, Nelson Mandela, J. K. Nyerere, Martin Luther King Jr n.k. Maono ndio yanayotengeneza makampuni, mashirika, taasisi, ajira kwa watu, biashara, miradi (projects) na sio kinyume chake. 
Ninaposema kila mtu ameitwa kuongoza sina maana kila mtu ameitwa kuwa mwanasiasa (wapo waliokusudiwa hapa pia); na wala si swala la kuwa na cheo au kutokuwa nacho! Bali kwa kuwa umeumbwa kwa kusudi fulani, inatosha kujua mahali uongozi wako unahitajika. Uongozi wako unaweza hitajika kwenye eneo la biashara, eneo la tekinolojia, eneo la sanaa na michezo, eneo la siasa, jamii (social leader), afya, uchumi au madhabahu! (Your area of gifting and passions)
Kwanini nasema umeitwa kuongoza? Kwa sababu maono hutolewa kwa mtu mmoja kwanza kabla hayajapata wafuasi wengi; Na pia kila mtu ana eneo au nafasi yake kwa kadri ya kusudi la kuumbwa kwako sawasawa na maono aliyonayo; Ni kwa sababu ulichopewa si kwa ajili yako, ni kwa ajili ya wengine (japo na wewe utanufaika), mfano. Mwalimu hawi mwalimu kwa ajili yake, japo hupokea malipo ya kazi hio!  Kumbuka, hakuna mti unakula matunda yake wenyewe!!
There's a place for you at the top

0 comments :