2018 Mwaka wa Masahihisho

8:44:00 PM Unknown 0 Comments

2018
MWAKA WA MASAHIHISHO
Kama wanadamu tunakosea na kila mwaka unatupa fursa ya kufanya mambo mawili mosi, unatupa fursa ya kufanya mambo mazuri na sahihi; pili, unatupa fursa ya kukosea. Amesema mzaburi, “BWANA kama wewe ungehesabu maovu yetu nani angesimama?” Kwa siku zaidi ya mia tatu za mwaka 2017 yako mengi yasiofaa ambayo tumeyatenda na hayapaswi kuendelea kufanyika; yako pia ya kufaa ambayo yanatakiwa kuendelezwa katika mwaka 2018. Yako pia mazuri ambayo tulitakiwa kufanya na hatukuyafanya!
Kwa kuwa katika mwaka 2017 kulikuwa na makosa na mapungufu ambayo kwa hekima ya kawaida huwa tunayachukua kama shule kwa ajili ya mwaka 2018 basi mapungufu hayo yasituumize. Hatutegemei katika mwaka 2018 kuendelea na makosa ya 2017 ambayo tumesha hitimu shule yake.
Tunaweza kutaka mabadiliko katika mwaka 2018 na tusiweze, pengine nguvu zetu ni kidogo na hutuwezi kugeuka, lakini uko msalaba na iko damu ya Yesu! Nguvu ile iliyohuisha mwili wake kaburini naye akafufuka mzima, yaweza kutuhuisha roho zetu na dhambi na kutufanya kuwa watu bora kabisa katika mwaka 2018. Najua nguvu zetu ni kidogo lakini panapo msalaba pana nguvu kubwa ya mageuzi.
Mamilioni ya watu wamekuwa wakipinduliwa kwa nguvu ya msalaba toka utumwa wa dhambi mpaka utakatifu. Nguvu hii ni kwa ajili yetu katika mwaka 2018. Kama tulikosea 2017 imetosha sasa, sasa tumejifunza, sasa ni wakati wa kugeuka. Moja na malengo yako katika mwaka 2018 ni muhimu kuwa kufanya yale uliyotakiwa kuyafanya katika mwaka 2017 na hukufanya. Hii pia ni lengo la kizazi cha sasa yaani, kufanya yale ambayo vizazi vilivyopita vilitakiwa kufanya na havikufanya. Mwalimu Jim Rohn amesema jambo la kufanana na somo hili, “Don’t let learning from your own experiences take too long. If you have been doing it wrong for the last ten years, I would suggest that’s long enough
Masahihisho ni jambo jema kabla ya hukumu, masahihisho yanatupa nafasi ya kujitathmini, kujikosoa na kuanza upya, kamwe yasitazamwe kama hukumu. Katika kitabu nikipendacho cha, “The Virgin Way” kilichoandikwa na Richard Branson imesisitizwa kama unafanya makosa na uyafanye haraka. Kipindi chako cha kukosea na kujifunza kutokana na makosa kisiwe kipindi kirefu mno. Hii imepelekea kukusihi, mwaka 2018 iwe muda wako wa kuanza upya. If you’re doing a mistake do it very quickly in these few days before 2018.
Tufikapo 2018 tuwe wapya tayari kwa ushindi.
Barikiwa!

0 comments :

Inachukua Muda....

5:32:00 PM Unknown 0 Comments

 
Inachukua Muda...

Tunaishi katika ulimwengu ambao karibu kila eneo watu hutaka huduma kwa haraka; usafiri wa haraka (mwendokasi), chakula cha haraka (fast food), mikopo ya haraka, huduma za kifedha na afya kwa haraka (fast track) n.k ! Hakuna anayetaka kukaa muda mrefu kwenye foleni kusubiria huduma. Maendeleo ya sayansi na tekinolojia yamerahisisha upatikana wa huduma nyingi katika jamii na kwa haraka zaidi wakati huu, kuliko miaka kumi iliyopita.
Pamoja na mchango mkubwa wa sayansi na tekinolojia katika upatikanaji wa huduma, watu wengi wamesahau baadhi ya kanuni muhimu za mafanikio ya kweli; katika ulimwengu huu wa haraka haraka, jamii imesahau kuwa mafanikio ya kudumu huchukua muda kuyajenga. Kanuni hii ni rahisi sana kusahaulika katika ulimwengu wa haraka.  Ya kwamba mahusiano mazuri yanachukua muda kuyajenga, familia nzuri inachukua muda kuijenga, mafanikio ya kifedha, huduma, taaluma pamoja na 'career' haya yote huchukua muda kuyajenga.
Ni mwanafunzi anayeamini katika ulimwengu wa haraka kwenye taalumu hufanya bidii aweze kuiba au kuibia kwenye mtihani, ni kijana anayeamini tu katika ulimwengu wa haraka hushinda kijiweni "akibeti" ili kufikia mafanikio ya kifedha. Ndio maana ni rahisi kwa mtu kwenda kucheza "desi" ili apokee mara asilimia mia tatu (300%) kuliko kuwekeza kwenye ufugaji wa kuku, kwa sababu anaona hatapata hiyo asilimia mia tatu haraka. Hutaka kupata kwa haraka bila kufanyia kazi. Nitajie tajiri aliyeko kwenye orodha ya matajiri kwa sababu alishida bahati nasibu au desi; go back to Work!!
Watu ambao hawajui kuwa mahusiano bora na imara huchukua muda kuyajenga wakitofautiana kidogo huvunja uhusiano huo na kama ni wana ndoa hutishia kutengana kabisa. Mzazi ambaye anayeamini katika ulimwengu wa haraka katika malezi, hana muda wa kukaa  na watoto kuwafundisha na kufuatilia malezi yao kwa karibu; wakishapotea na kuharibika kimwenendo hukimbilia kwa watumishi wamuombee ili wapone na kurudi kwenye njia sahihi kwa haraka, amesahau alikuwa na nafasi katika kujenga mwenendo bora kabla.
Anayejenga nyumba juu ya mwamba hutumia muda kuijenga, na kwa sababu hiyo nyumba hiyo itakuwa imara kuliko anayejenga juu ya mchanga.  Kuna baadhi ya maeneo ulimwengu wa haraka hauleti matokeo bora, bali kanuni ya muda!  Mwenyehekima mmoja amewahi kusema "usikimbie mahali panapokutaka kutembea; na usitembee mahali panapokutaka kukimbia "
Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa-Mithali 13 :11
There's a place for you at the top

0 comments :